Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

83 Al-Muţaffifīn ٱلْمُطَفِّفِين

< Previous   36 Āyah   The Defrauding      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

83:1 وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ
83:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ole wao hao wapunjao!

83:2 ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ
83:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

83:3 وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ
83:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

83:4 أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَـٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ
83:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

83:5 لِيَوْمٍ عَظِيمٍ
83:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika Siku iliyo kuu,

83:6 يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
83:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

83:7 كَلَّآ إِنَّ كِتَـٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍ
83:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

83:8 وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌ
83:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Unajua nini Sijjin?

83:9 كِتَـٰبٌ مَّرْقُومٌ
83:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kitabu kilicho andikwa.

83:10 وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
83:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

83:11 ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
83:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

83:12 وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
83:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

83:13 إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَـٰتُنَا قَالَ أَسَـٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ
83:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

83:14 كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
83:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

83:15 كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ
83:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

83:16 ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ
83:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha wataingia Motoni!

83:17 ثُمَّ يُقَالُ هَـٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
83:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

83:18 كَلَّآ إِنَّ كِتَـٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ
83:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

83:19 وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ
83:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

83:20 كِتَـٰبٌ مَّرْقُومٌ
83:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kitabu kilicho andikwa.

83:21 يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ
83:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanakishuhudia walio karibishwa.

83:22 إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ
83:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

83:23 عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
83:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

83:24 تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ
83:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

83:25 يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ
83:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

83:26 خِتَـٰمُهُۥ مِسْكٌ ۚ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَـٰفِسُونَ
83:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

83:27 وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ
83:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

83:28 عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ
83:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

83:29 إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ
83:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

83:30 وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ
83:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

83:31 وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ
83:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

83:32 وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ
83:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

83:33 وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَـٰفِظِينَ
83:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

83:34 فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ
83:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

83:35 عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
83:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

83:36 هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ
83:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?