Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

37 Aş-Şāffāt ٱلصَّافَّات

< Previous   182 Āyah   Those who set the Ranks      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

37:1 وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفًّا
37:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.

37:2 فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًا
37:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa wenye kukataza mabaya.

37:3 فَٱلتَّـٰلِيَـٰتِ ذِكْرًا
37:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

37:4 إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌ
37:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

37:5 رَّبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَـٰرِقِ
37:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

37:6 إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ
37:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.

37:7 وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ مَّارِدٍ
37:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kulinda na kila shet'ani a'si.

37:8 لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
37:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

37:9 دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
37:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

37:10 إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
37:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.

37:11 فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍۭ
37:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.

37:12 بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
37:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

37:13 وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ
37:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.

37:14 وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةً يَسْتَسْخِرُونَ
37:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.

37:15 وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
37:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.

37:16 أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
37:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

37:17 أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
37:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hata baba zetu wa zamani?

37:18 قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ
37:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.

37:19 فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
37:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!

37:20 وَقَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَا هَـٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
37:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

37:21 هَـٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
37:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.

37:22 ۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ
37:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -

37:23 مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ
37:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

37:24 وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ
37:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:

37:25 مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
37:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mna nini? Mbona hamsaidiani?

37:26 بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
37:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bali hii leo, watasalimu amri.

37:27 وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
37:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.

37:28 قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ
37:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.

37:29 قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
37:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.

37:30 وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَـٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَـٰغِينَ
37:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.

37:31 فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
37:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

37:32 فَأَغْوَيْنَـٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَـٰوِينَ
37:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

37:33 فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
37:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.

37:34 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
37:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.

37:35 إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
37:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.

37:36 وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍۭ
37:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?

37:37 بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.

37:38 إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ
37:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.

37:39 وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
37:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.

37:40 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

37:41 أُو۟لَـٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
37:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,

37:42 فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
37:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Matunda, nao watahishimiwa.

37:43 فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
37:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika Bustani za neema.

37:44 عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ
37:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wako juu ya viti wamekabiliana.

37:45 يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍۭ
37:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem

37:46 بَيْضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّـٰرِبِينَ
37:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.

37:47 لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
37:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

37:48 وَعِندَهُمْ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌ
37:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.

37:49 كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
37:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.

37:50 فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
37:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.

37:51 قَالَ قَآئِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌ
37:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki

37:52 يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ
37:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki

37:53 أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
37:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?

37:54 قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
37:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Atasema: Je! Nyie mnawaona?

37:55 فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
37:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.

37:56 قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
37:56
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.

37:57 وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ
37:57
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.

37:58 أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
37:58
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Sisi hatutakufa,

37:59 إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
37:59
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.

37:60 إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
37:60
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.

37:61 لِمِثْلِ هَـٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَـٰمِلُونَ
37:61
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.

37:62 أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
37:62
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?

37:63 إِنَّا جَعَلْنَـٰهَا فِتْنَةً لِّلظَّـٰلِمِينَ
37:63
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.

37:64 إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ
37:64
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.

37:65 طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَـٰطِينِ
37:65
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.

37:66 فَإِنَّهُمْ لَـَٔاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
37:66
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.

37:67 ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
37:67
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.

37:68 ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ
37:68
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.

37:69 إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ
37:69
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.

37:70 فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَـٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ
37:70
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.

37:71 وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ
37:71
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.

37:72 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
37:72
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.

37:73 فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَـٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ
37:73
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.

37:74 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:74
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

37:75 وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ
37:75
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.

37:76 وَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
37:76
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.

37:77 وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ
37:77
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.

37:78 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:78
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.

37:79 سَلَـٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِى ٱلْعَـٰلَمِينَ
37:79
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!

37:80 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:80
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

37:81 إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:81
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

37:82 ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
37:82
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha tukawazamisha wale wengine.

37:83 ۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ
37:83
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,

37:84 إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
37:84
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.

37:85 إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ
37:85
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?

37:86 أَئِفْكًا ءَالِهَةً دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
37:86
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?

37:87 فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
37:87
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?

37:88 فَنَظَرَ نَظْرَةً فِى ٱلنُّجُومِ
37:88
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.

37:89 فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌ
37:89
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!

37:90 فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ
37:90
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.

37:91 فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
37:91
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?

37:92 مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
37:92
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mna nini hata hamsemi?

37:93 فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ
37:93
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.

37:94 فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
37:94
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wakamjia upesi upesi.

37:95 قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
37:95
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?

37:96 وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
37:96
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!

37:97 قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَـٰنًا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ
37:97
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!

37:98 فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًا فَجَعَلْنَـٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ
37:98
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.

37:99 وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ
37:99
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

37:100 رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
37:100
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

37:101 فَبَشَّرْنَـٰهُ بِغُلَـٰمٍ حَلِيمٍ
37:101
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

37:102 فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَـٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَـٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّـٰبِرِينَ
37:102
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.

37:103 فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ
37:103
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

37:104 وَنَـٰدَيْنَـٰهُ أَن يَـٰٓإِبْرَٰهِيمُ
37:104
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tulimwita: Ewe Ibrahim!

37:105 قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:105
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.

37:106 إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَـٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ
37:106
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.

37:107 وَفَدَيْنَـٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
37:107
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.

37:108 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:108
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.

37:109 سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ
37:109
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Iwe salama kwa Ibrahim!

37:110 كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:110
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

37:111 إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:111
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

37:112 وَبَشَّرْنَـٰهُ بِإِسْحَـٰقَ نَبِيًّا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
37:112
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.

37:113 وَبَـٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَـٰقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌ
37:113
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.

37:114 وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
37:114
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.

37:115 وَنَجَّيْنَـٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
37:115
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.

37:116 وَنَصَرْنَـٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
37:116
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.

37:117 وَءَاتَيْنَـٰهُمَا ٱلْكِتَـٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ
37:117
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.

37:118 وَهَدَيْنَـٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
37:118
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.

37:119 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:119
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.

37:120 سَلَـٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
37:120
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Iwe salama kwa Musa na Haruni!

37:121 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:121
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.

37:122 إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:122
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.

37:123 وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:123
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

37:124 إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
37:124
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?

37:125 أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَـٰلِقِينَ
37:125
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,

37:126 ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
37:126
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?

37:127 فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
37:127
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;

37:128 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:128
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.

37:129 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:129
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.

37:130 سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ
37:130
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Iwe salama kwa Ilyas.

37:131 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:131
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.

37:132 إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:132
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

37:133 وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:133
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

37:134 إِذْ نَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
37:134
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,

37:135 إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
37:135
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.

37:136 ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
37:136
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.

37:137 وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
37:137
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,

37:138 وَبِٱلَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
37:138
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?

37:139 وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:139
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.

37:140 إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
37:140
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.

37:141 فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ
37:141
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.

37:142 فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ
37:142
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.

37:143 فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ
37:143
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,

37:144 لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
37:144
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.

37:145 ۞ فَنَبَذْنَـٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌ
37:145
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.

37:146 وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ
37:146
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.

37:147 وَأَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
37:147
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.

37:148 فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَـٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍ
37:148
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

37:149 فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ
37:149
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?

37:150 أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ إِنَـٰثًا وَهُمْ شَـٰهِدُونَ
37:150
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

37:151 أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
37:151
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:

37:152 وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَـٰذِبُونَ
37:152
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!

37:153 أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ
37:153
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?

37:154 مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
37:154
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?

37:155 أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
37:155
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hamkumbuki?

37:156 أَمْ لَكُمْ سُلْطَـٰنٌ مُّبِينٌ
37:156
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Au mnayo hoja iliyo wazi?

37:157 فَأْتُوا۟ بِكِتَـٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
37:157
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.

37:158 وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
37:158
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

37:159 سُبْحَـٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
37:159
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.

37:160 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:160
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.

37:161 فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
37:161
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu

37:162 مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَـٰتِنِينَ
37:162
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hamwezi kuwapoteza

37:163 إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ
37:163
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.

37:164 وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ
37:164
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.

37:165 وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ
37:165
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

37:166 وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ
37:166
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.

37:167 وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ
37:167
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:

37:168 لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
37:168
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,

37:169 لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:169
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.

37:170 فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
37:170
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.

37:171 وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ
37:171
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.

37:172 إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ
37:172
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.

37:173 وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
37:173
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.

37:174 فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
37:174
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi waachilie mbali kwa muda.

37:175 وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
37:175
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watazame, nao wataona.

37:176 أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
37:176
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?

37:177 فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ
37:177
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.

37:178 وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
37:178
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na waache kwa muda.

37:179 وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
37:179
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tazama, na wao wataona.

37:180 سُبْحَـٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
37:180
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.

37:181 وَسَلَـٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ
37:181
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Salamu juu ya Mitume.

37:182 وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
37:182
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.