Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

89 Al-Fajr ٱلْفَجْر

< Previous   30 Āyah   The Dawn      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

89:1 وَٱلْفَجْرِ
89:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa alfajiri,

89:2 وَلَيَالٍ عَشْرٍ
89:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa masiku kumi,

89:3 وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ
89:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

89:4 وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ
89:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa usiku unapo pita,

89:5 هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِى حِجْرٍ
89:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

89:6 أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
89:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

89:7 إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ
89:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wa Iram, wenye majumba marefu?

89:8 ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَـٰدِ
89:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

89:9 وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ
89:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

89:10 وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ
89:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Firauni mwenye vigingi?

89:11 ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَـٰدِ
89:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao walifanya jeuri katika nchi?

89:12 فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ
89:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakakithirisha humo ufisadi?

89:13 فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ
89:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

89:14 إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ
89:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

89:15 فَأَمَّا ٱلْإِنسَـٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ
89:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

89:16 وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَـٰنَنِ
89:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

89:17 كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ
89:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

89:18 وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
89:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala hamhimizani kulisha masikini;

89:19 وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا
89:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

89:20 وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّا جَمًّا
89:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

89:21 كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا
89:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

89:22 وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
89:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

89:23 وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَـٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ
89:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

89:24 يَقُولُ يَـٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى
89:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

89:25 فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌ
89:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

89:26 وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌ
89:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

89:27 يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ
89:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ewe nafsi iliyo tua!

89:28 ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً
89:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

89:29 فَٱدْخُلِى فِى عِبَـٰدِى
89:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

89:30 وَٱدْخُلِى جَنَّتِى
89:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ingia katika Pepo yangu.