Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

26 Ash-Shu`arā' ٱلشُّعَرَاء

< Previous   227 Āyah   The Poets      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

26:1 طسٓمٓ
26:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)

26:2 تِلْكَ ءَايَـٰتُ ٱلْكِتَـٰبِ ٱلْمُبِينِ
26:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

26:3 لَعَلَّكَ بَـٰخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
26:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

26:4 إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةً فَظَلَّتْ أَعْنَـٰقُهُمْ لَهَا خَـٰضِعِينَ
26:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.

26:5 وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ ٱلرَّحْمَـٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ
26:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.

26:6 فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَـٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
26:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.

26:7 أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
26:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

26:8 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

26:9 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:10 وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
26:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,

26:11 قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ
26:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watu wa Firauni. Hawaogopi?

26:12 قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
26:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.

26:13 وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَـٰرُونَ
26:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

26:14 وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
26:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.

26:15 قَالَ كَلَّا ۖ فَٱذْهَبَا بِـَٔايَـٰتِنَآ ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
26:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

26:16 فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:17 أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.

26:18 قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
26:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?

26:19 وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَـٰفِرِينَ
26:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?

26:20 قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
26:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.

26:21 فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

26:22 وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

26:23 قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

26:24 قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
26:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

26:25 قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
26:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?

26:26 قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
26:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

26:27 قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
26:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.

26:28 قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ
26:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

26:29 قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَـٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ
26:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

26:30 قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍ مُّبِينٍ
26:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

26:31 قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
26:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.

26:32 فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
26:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.

26:33 وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ
26:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.

26:34 قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَـٰذَا لَسَـٰحِرٌ عَلِيمٌ
26:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

26:35 يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
26:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

26:36 قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ
26:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.

26:37 يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
26:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

26:38 فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
26:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.

26:39 وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
26:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?

26:40 لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
26:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.

26:41 فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
26:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?

26:42 قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
26:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

26:43 قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ
26:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.

26:44 فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
26:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

26:45 فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
26:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.

26:46 فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَـٰجِدِينَ
26:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.

26:47 قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:48 رَبِّ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
26:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mola Mlezi wa Musa na Harun.

26:49 قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَـٰفٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
26:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.

26:50 قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
26:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

26:51 إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَـٰيَـٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.

26:52 ۞ وَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِىٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
26:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

26:53 فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ
26:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.

26:54 إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
26:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

26:55 وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَآئِظُونَ
26:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nao wanatuudhi.

26:56 وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَـٰذِرُونَ
26:56
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.

26:57 فَأَخْرَجْنَـٰهُم مِّن جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
26:57
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,

26:58 وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
26:58
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na makhazina, na vyeo vya hishima,

26:59 كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَـٰهَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:59
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

26:60 فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
26:60
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.

26:61 فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَـٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
26:61
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!

26:62 قَالَ كَلَّآ ۖ إِنَّ مَعِىَ رَبِّى سَيَهْدِينِ
26:62
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

26:63 فَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضْرِب بِّعَصَاكَ ٱلْبَحْرَ ۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَٱلطَّوْدِ ٱلْعَظِيمِ
26:63
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

26:64 وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ ٱلْـَٔاخَرِينَ
26:64
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawajongeza hapo wale wengine.

26:65 وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
26:65
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.

26:66 ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
26:66
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha tukawazamisha hao wengine.

26:67 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:67
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.

26:68 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:68
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:69 وَٱتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَٰهِيمَ
26:69
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wasomee khabari za Ibrahim.

26:70 إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَا تَعْبُدُونَ
26:70
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

26:71 قَالُوا۟ نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَـٰكِفِينَ
26:71
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

26:72 قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
26:72
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?

26:73 أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
26:73
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?

26:74 قَالُوا۟ بَلْ وَجَدْنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
26:74
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

26:75 قَالَ أَفَرَءَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
26:75
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-

26:76 أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلْأَقْدَمُونَ
26:76
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nyinyi na baba zenu wa zamani?

26:77 فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّىٓ إِلَّا رَبَّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:77
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:78 ٱلَّذِى خَلَقَنِى فَهُوَ يَهْدِينِ
26:78
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,

26:79 وَٱلَّذِى هُوَ يُطْعِمُنِى وَيَسْقِينِ
26:79
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

26:80 وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
26:80
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.

26:81 وَٱلَّذِى يُمِيتُنِى ثُمَّ يُحْيِينِ
26:81
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

26:82 وَٱلَّذِىٓ أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِى خَطِيٓـَٔتِى يَوْمَ ٱلدِّينِ
26:82
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

26:83 رَبِّ هَبْ لِى حُكْمًا وَأَلْحِقْنِى بِٱلصَّـٰلِحِينَ
26:83
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.

26:84 وَٱجْعَل لِّى لِسَانَ صِدْقٍ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
26:84
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.

26:85 وَٱجْعَلْنِى مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
26:85
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

26:86 وَٱغْفِرْ لِأَبِىٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
26:86
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

26:87 وَلَا تُخْزِنِى يَوْمَ يُبْعَثُونَ
26:87
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.

26:88 يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
26:88
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.

26:89 إِلَّا مَنْ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
26:89
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.

26:90 وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
26:90
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.

26:91 وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
26:91
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

26:92 وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
26:92
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu

26:93 مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
26:93
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?

26:94 فَكُبْكِبُوا۟ فِيهَا هُمْ وَٱلْغَاوُۥنَ
26:94
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,

26:95 وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
26:95
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na majeshi ya Ibilisi yote.

26:96 قَالُوا۟ وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
26:96
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

26:97 تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِى ضَلَـٰلٍ مُّبِينٍ
26:97
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,

26:98 إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:98
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:99 وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلْمُجْرِمُونَ
26:99
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.

26:100 فَمَا لَنَا مِن شَـٰفِعِينَ
26:100
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hatuna waombezi.

26:101 وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
26:101
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala rafiki wa dhati.

26:102 فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:102
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.

26:103 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:103
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

26:104 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:104
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:105 كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:105
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

26:106 إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:106
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?

26:107 إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:107
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

26:108 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:108
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

26:109 وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:109
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:110 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:110
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

26:111 ۞ قَالُوٓا۟ أَنُؤْمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلْأَرْذَلُونَ
26:111
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?

26:112 قَالَ وَمَا عِلْمِى بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
26:112
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?

26:113 إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّى ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
26:113
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!

26:114 وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:114
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

26:115 إِنْ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
26:115
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.

26:116 قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَـٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمَرْجُومِينَ
26:116
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

26:117 قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِى كَذَّبُونِ
26:117
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.

26:118 فَٱفْتَحْ بَيْنِى وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِى وَمَن مَّعِىَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:118
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

26:119 فَأَنجَيْنَـٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
26:119
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.

26:120 ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ ٱلْبَاقِينَ
26:120
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

26:121 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:121
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.

26:122 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:122
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:123 كَذَّبَتْ عَادٌ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:123
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kina A'd waliwakanusha Mitume.

26:124 إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:124
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?

26:125 إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:125
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

26:126 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:126
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

26:127 وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:127
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:128 أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةً تَعْبَثُونَ
26:128
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

26:129 وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ
26:129
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!

26:130 وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ
26:130
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.

26:131 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:131
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

26:132 وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِىٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ
26:132
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

26:133 أَمَدَّكُم بِأَنْعَـٰمٍ وَبَنِينَ
26:133
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.

26:134 وَجَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
26:134
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mabustani na chemchem.

26:135 إِنِّىٓ أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
26:135
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.

26:136 قَالُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْنَآ أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ ٱلْوَٰعِظِينَ
26:136
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

26:137 إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلْأَوَّلِينَ
26:137
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

26:138 وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
26:138
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala sisi hatutaadhibiwa.

26:139 فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَـٰهُمْ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:139
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

26:140 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:140
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:141 كَذَّبَتْ ثَمُودُ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:141
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.

26:142 إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَـٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:142
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?

26:143 إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:143
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

26:144 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:144
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

26:145 وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:145
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:146 أَتُتْرَكُونَ فِى مَا هَـٰهُنَآ ءَامِنِينَ
26:146
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?

26:147 فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
26:147
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika mabustani, na chemchem?

26:148 وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ
26:148
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.

26:149 وَتَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًا فَـٰرِهِينَ
26:149
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

26:150 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:150
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

26:151 وَلَا تُطِيعُوٓا۟ أَمْرَ ٱلْمُسْرِفِينَ
26:151
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,

26:152 ٱلَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
26:152
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.

26:153 قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
26:153
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.

26:154 مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
26:154
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

26:155 قَالَ هَـٰذِهِۦ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
26:155
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

26:156 وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ
26:156
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.

26:157 فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا۟ نَـٰدِمِينَ
26:157
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.

26:158 فَأَخَذَهُمُ ٱلْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:158
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

26:159 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:159
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:160 كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:160
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.

26:161 إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:161
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?

26:162 إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:162
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.

26:163 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:163
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

26:164 وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:164
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:165 أَتَأْتُونَ ٱلذُّكْرَانَ مِنَ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:165
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

26:166 وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَٰجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ
26:166
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!

26:167 قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَـٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمُخْرَجِينَ
26:167
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!

26:168 قَالَ إِنِّى لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلْقَالِينَ
26:168
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.

26:169 رَبِّ نَجِّنِى وَأَهْلِى مِمَّا يَعْمَلُونَ
26:169
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

26:170 فَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
26:170
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,

26:171 إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
26:171
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.

26:172 ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
26:172
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha tukawaangamiza wale wengine.

26:173 وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلْمُنذَرِينَ
26:173
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.

26:174 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:174
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

26:175 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:175
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

26:176 كَذَّبَ أَصْحَـٰبُ لْـَٔيْكَةِ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:176
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

26:177 إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:177
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?

26:178 إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:178
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

26:179 فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:179
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

26:180 وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:180
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:181 ۞ أَوْفُوا۟ ٱلْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا۟ مِنَ ٱلْمُخْسِرِينَ
26:181
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.

26:182 وَزِنُوا۟ بِٱلْقِسْطَاسِ ٱلْمُسْتَقِيمِ
26:182
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;

26:183 وَلَا تَبْخَسُوا۟ ٱلنَّاسَ أَشْيَآءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا۟ فِى ٱلْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
26:183
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.

26:184 وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِى خَلَقَكُمْ وَٱلْجِبِلَّةَ ٱلْأَوَّلِينَ
26:184
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.

26:185 قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
26:185
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.

26:186 وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلْكَـٰذِبِينَ
26:186
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

26:187 فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
26:187
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

26:188 قَالَ رَبِّىٓ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
26:188
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.

26:189 فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ ٱلظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
26:189
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

26:190 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:190
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

26:191 وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:191
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:192 وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:192
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

26:193 نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلْأَمِينُ
26:193
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ameuteremsha Roho muaminifu,

26:194 عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُنذِرِينَ
26:194
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,

26:195 بِلِسَانٍ عَرَبِىٍّ مُّبِينٍ
26:195
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.

26:196 وَإِنَّهُۥ لَفِى زُبُرِ ٱلْأَوَّلِينَ
26:196
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

26:197 أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ ءَايَةً أَن يَعْلَمَهُۥ عُلَمَـٰٓؤُا۟ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:197
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?

26:198 وَلَوْ نَزَّلْنَـٰهُ عَلَىٰ بَعْضِ ٱلْأَعْجَمِينَ
26:198
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,

26:199 فَقَرَأَهُۥ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا۟ بِهِۦ مُؤْمِنِينَ
26:199
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.

26:200 كَذَٰلِكَ سَلَكْنَـٰهُ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ
26:200
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

26:201 لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُا۟ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
26:201
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

26:202 فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
26:202
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.

26:203 فَيَقُولُوا۟ هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ
26:203
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watasema: Je, tutapewa muhula?

26:204 أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
26:204
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?

26:205 أَفَرَءَيْتَ إِن مَّتَّعْنَـٰهُمْ سِنِينَ
26:205
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,

26:206 ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
26:206
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,

26:207 مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يُمَتَّعُونَ
26:207
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?

26:208 وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
26:208
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -

26:209 ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَـٰلِمِينَ
26:209
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

26:210 وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ ٱلشَّيَـٰطِينُ
26:210
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,

26:211 وَمَا يَنۢبَغِى لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
26:211
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

26:212 إِنَّهُمْ عَنِ ٱلسَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
26:212
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hao wametengwa na kusikia.

26:213 فَلَا تَدْعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلْمُعَذَّبِينَ
26:213
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.

26:214 وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ ٱلْأَقْرَبِينَ
26:214
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

26:215 وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:215
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.

26:216 فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّى بَرِىٓءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ
26:216
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.

26:217 وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
26:217
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

26:218 ٱلَّذِى يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
26:218
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambaye anakuona unapo simama,

26:219 وَتَقَلُّبَكَ فِى ٱلسَّـٰجِدِينَ
26:219
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.

26:220 إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ
26:220
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.

26:221 هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَـٰطِينُ
26:221
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?

26:222 تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ
26:222
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

26:223 يُلْقُونَ ٱلسَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَـٰذِبُونَ
26:223
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.

26:224 وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلْغَاوُۥنَ
26:224
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.

26:225 أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِى كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ
26:225
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

26:226 وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ
26:226
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?

26:227 إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ وَذَكَرُوا۟ ٱللَّهَ كَثِيرًا وَٱنتَصَرُوا۟ مِنۢ بَعْدِ مَا ظُلِمُوا۟ ۗ وَسَيَعْلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓا۟ أَىَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ
26:227
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.