Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

88 Al-Ghāshiyah ٱلْغَاشِيَة

< Previous   26 Āyah   The Overwhelming      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

88:1 هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَـٰشِيَةِ
88:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

88:2 وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَـٰشِعَةٌ
88:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku hiyo nyuso zitainama,

88:3 عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ
88:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Zikifanya kazi, nazo taabani.

88:4 تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً
88:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ziingie katika Moto unao waka -

88:5 تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍ
88:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

88:6 لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ
88:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

88:7 لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍ
88:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

88:8 وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ
88:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

88:9 لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ
88:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

88:10 فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍ
88:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika Bustani ya juu.

88:11 لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَـٰغِيَةً
88:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hawatasikia humo upuuzi.

88:12 فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ
88:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo imo chemchem inayo miminika.

88:13 فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ
88:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

88:14 وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ
88:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bilauri zilizo pangwa,

88:15 وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ
88:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na matakia safu safu,

88:16 وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ
88:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mazulia yaliyo tandikwa.

88:17 أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
88:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

88:18 وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
88:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

88:19 وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
88:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

88:20 وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
88:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

88:21 فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌ
88:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

88:22 لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
88:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wewe si mwenye kuwatawalia.

88:23 إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
88:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

88:24 فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ
88:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

88:25 إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ
88:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

88:26 ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
88:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!