Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

37 Aş-Şāffāt ٱلصَّافَّات

< Previous   182 Āyah   Those who set the Ranks      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

37:1 وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفًّا
37:1 Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:2 فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًا
37:2 Na kwa wenye kukataza mabaya. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:3 فَٱلتَّـٰلِيَـٰتِ ذِكْرًا
37:3 Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:4 إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌ
37:4 Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:5 رَّبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَـٰرِقِ
37:5 Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:6 إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ
37:6 Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:7 وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ مَّارِدٍ
37:7 Na kulinda na kila shet'ani a'si. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:8 لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
37:8 Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:9 دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
37:9 Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:10 إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
37:10 Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:11 فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍۭ
37:11 Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:12 بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
37:12 Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:13 وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ
37:13 Na wanapo kumbushwa hawakumbuki. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:14 وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةً يَسْتَسْخِرُونَ
37:14 Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:15 وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
37:15 Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:16 أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
37:16 Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:17 أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
37:17 Hata baba zetu wa zamani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:18 قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ
37:18 Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:19 فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
37:19 Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:20 وَقَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَا هَـٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
37:20 Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:21 هَـٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
37:21 Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:22 ۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ
37:22 Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu - - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:23 مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ
37:23 Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:24 وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ
37:24 Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa: - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:25 مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
37:25 Mna nini? Mbona hamsaidiani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:26 بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
37:26 Bali hii leo, watasalimu amri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:27 وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
37:27 Watakabiliana wao kwa wao kuulizana. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:28 قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ
37:28 Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:29 قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
37:29 Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:30 وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَـٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَـٰغِينَ
37:30 Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:31 فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
37:31 Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:32 فَأَغْوَيْنَـٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَـٰوِينَ
37:32 Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:33 فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
37:33 Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:34 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
37:34 Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:35 إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
37:35 Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:36 وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍۭ
37:36 Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:37 بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:37 Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:38 إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ
37:38 Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:39 وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
37:39 Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:40 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:40 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:41 أُو۟لَـٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
37:41 Hao ndio watakao pata riziki maalumu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:42 فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
37:42 Matunda, nao watahishimiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:43 فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
37:43 Katika Bustani za neema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:44 عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ
37:44 Wako juu ya viti wamekabiliana. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:45 يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍۭ
37:45 Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:46 بَيْضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّـٰرِبِينَ
37:46 Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:47 لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
37:47 Hakina madhara, wala hakiwaleweshi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:48 وَعِندَهُمْ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌ
37:48 Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:49 كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
37:49 Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:50 فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
37:50 Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:51 قَالَ قَآئِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌ
37:51 Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:52 يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ
37:52 Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:53 أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
37:53 Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:54 قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
37:54 Atasema: Je! Nyie mnawaona? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:55 فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
37:55 Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:56 قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
37:56 Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:57 وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ
37:57 Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:58 أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
37:58 Je! Sisi hatutakufa, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:59 إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
37:59 Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:60 إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
37:60 Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:61 لِمِثْلِ هَـٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَـٰمِلُونَ
37:61 Kwa mfano wa haya nawatende watendao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:62 أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
37:62 Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:63 إِنَّا جَعَلْنَـٰهَا فِتْنَةً لِّلظَّـٰلِمِينَ
37:63 Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:64 إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ
37:64 Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:65 طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَـٰطِينِ
37:65 Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:66 فَإِنَّهُمْ لَـَٔاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
37:66 Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:67 ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
37:67 Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:68 ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ
37:68 Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:69 إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ
37:69 Hakika waliwakuta baba zao wamepotea. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:70 فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَـٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ
37:70 Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:71 وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ
37:71 Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:72 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
37:72 Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:73 فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَـٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ
37:73 Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:74 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:74 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:75 وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ
37:75 Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:76 وَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
37:76 Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:77 وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ
37:77 Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:78 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:78 Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:79 سَلَـٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِى ٱلْعَـٰلَمِينَ
37:79 Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:80 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:80 Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:81 إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:81 Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:82 ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
37:82 Kisha tukawazamisha wale wengine. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:83 ۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ
37:83 Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:84 إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
37:84 Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:85 إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ
37:85 Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:86 أَئِفْكًا ءَالِهَةً دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
37:86 Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:87 فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
37:87 Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:88 فَنَظَرَ نَظْرَةً فِى ٱلنُّجُومِ
37:88 Kisha akapiga jicho kutazama nyota. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:89 فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌ
37:89 Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:90 فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ
37:90 Nao wakamwacha, wakampa kisogo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:91 فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
37:91 Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:92 مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
37:92 Mna nini hata hamsemi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:93 فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ
37:93 Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:94 فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
37:94 Basi wakamjia upesi upesi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:95 قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
37:95 Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:96 وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
37:96 Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:97 قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَـٰنًا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ
37:97 Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:98 فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًا فَجَعَلْنَـٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ
37:98 Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:99 وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ
37:99 Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:100 رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
37:100 Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:101 فَبَشَّرْنَـٰهُ بِغُلَـٰمٍ حَلِيمٍ
37:101 Basi tukambashiria mwana aliye mpole. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:102 فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَـٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَـٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّـٰبِرِينَ
37:102 Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:103 فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ
37:103 Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:104 وَنَـٰدَيْنَـٰهُ أَن يَـٰٓإِبْرَٰهِيمُ
37:104 Tulimwita: Ewe Ibrahim! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:105 قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:105 Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:106 إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَـٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ
37:106 Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:107 وَفَدَيْنَـٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
37:107 Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:108 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:108 Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:109 سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ
37:109 Iwe salama kwa Ibrahim! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:110 كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:110 Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:111 إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:111 Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:112 وَبَشَّرْنَـٰهُ بِإِسْحَـٰقَ نَبِيًّا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
37:112 Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:113 وَبَـٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَـٰقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌ
37:113 Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:114 وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
37:114 Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:115 وَنَجَّيْنَـٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
37:115 Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:116 وَنَصَرْنَـٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
37:116 Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:117 وَءَاتَيْنَـٰهُمَا ٱلْكِتَـٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ
37:117 Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:118 وَهَدَيْنَـٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
37:118 Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:119 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:119 Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:120 سَلَـٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
37:120 Iwe salama kwa Musa na Haruni! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:121 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:121 Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:122 إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:122 Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:123 وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:123 Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:124 إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
37:124 Alipo waambia watu wake: Hamwogopi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:125 أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَـٰلِقِينَ
37:125 Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:126 ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
37:126 Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:127 فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
37:127 Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa; - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:128 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:128 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:129 وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
37:129 Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:130 سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ
37:130 Iwe salama kwa Ilyas. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:131 إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
37:131 Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:132 إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
37:132 Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:133 وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:133 Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:134 إِذْ نَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
37:134 Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:135 إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
37:135 Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:136 ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
37:136 Kisha tukawaangamiza wale wengineo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:137 وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
37:137 Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:138 وَبِٱلَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
37:138 Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:139 وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
37:139 Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:140 إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
37:140 Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:141 فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ
37:141 Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:142 فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ
37:142 Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:143 فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ
37:143 Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:144 لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
37:144 Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:145 ۞ فَنَبَذْنَـٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌ
37:145 Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:146 وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ
37:146 Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:147 وَأَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
37:147 Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:148 فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَـٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍ
37:148 Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:149 فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ
37:149 Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:150 أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ إِنَـٰثًا وَهُمْ شَـٰهِدُونَ
37:150 Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:151 أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
37:151 Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema: - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:152 وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَـٰذِبُونَ
37:152 Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:153 أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ
37:153 Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:154 مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
37:154 Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:155 أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
37:155 Hamkumbuki? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:156 أَمْ لَكُمْ سُلْطَـٰنٌ مُّبِينٌ
37:156 Au mnayo hoja iliyo wazi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:157 فَأْتُوا۟ بِكِتَـٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
37:157 Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:158 وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
37:158 Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:159 سُبْحَـٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
37:159 Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:160 إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:160 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:161 فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
37:161 Basi hakika nyinyi na mnao waabudu - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:162 مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَـٰتِنِينَ
37:162 Hamwezi kuwapoteza - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:163 إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ
37:163 Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:164 وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ
37:164 Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:165 وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ
37:165 Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:166 وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ
37:166 Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:167 وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ
37:167 Na walikuwapo walio kuwa wakisema: - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:168 لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
37:168 Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:169 لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
37:169 Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:170 فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
37:170 Lakini waliukataa. Basi watakuja jua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:171 وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ
37:171 Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:172 إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ
37:172 Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:173 وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
37:173 Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:174 فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
37:174 Basi waachilie mbali kwa muda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:175 وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
37:175 Na watazame, nao wataona. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:176 أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
37:176 Je! Wanaihimiza adhabu yetu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:177 فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ
37:177 Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:178 وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
37:178 Na waache kwa muda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:179 وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
37:179 Na tazama, na wao wataona. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:180 سُبْحَـٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
37:180 Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:181 وَسَلَـٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ
37:181 Na Salamu juu ya Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)

37:182 وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
37:182 Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)