Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

70 Al-Ma`ārij ٱلْمَعَارِج

< Previous   44 Āyah   The Ascending Stairways      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

70:1 سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ
70:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,

70:2 لِّلْكَـٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌ
70:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -

70:3 مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ
70:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

70:4 تَعْرُجُ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ
70:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!

70:5 فَٱصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا
70:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi subiri kwa subira njema.

70:6 إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًا
70:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wao wanaiona iko mbali,

70:7 وَنَرَىٰهُ قَرِيبًا
70:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Sisi tunaiona iko karibu.

70:8 يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ
70:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.

70:9 وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ
70:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na milima itakuwa kama sufi.

70:10 وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا
70:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

70:11 يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ
70:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,

70:12 وَصَـٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ
70:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mkewe, na nduguye,

70:13 وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ
70:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,

70:14 وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ
70:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

70:15 كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
70:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

70:16 نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ
70:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Unao babua ngozi ya kichwa!

70:17 تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ
70:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.

70:18 وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ
70:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

70:19 ۞ إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا
70:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mtu ameumbwa na papara.

70:20 إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًا
70:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Inapo mgusa shari hupapatika.

70:21 وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا
70:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na inapo mgusa kheri huizuilia.

70:22 إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ
70:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa wanao sali,

70:23 ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ
70:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao wanadumisha Sala zao,

70:24 وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ
70:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

70:25 لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
70:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;

70:26 وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
70:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

70:27 وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ
70:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

70:28 إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ
70:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.

70:29 وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَـٰفِظُونَ
70:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao wanahifadhi tupu zao.

70:30 إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَـٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
70:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -

70:31 فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ
70:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.

70:32 وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَـٰنَـٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ
70:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

70:33 وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَـٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ
70:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

70:34 وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
70:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

70:35 أُو۟لَـٰٓئِكَ فِى جَنَّـٰتٍ مُّكْرَمُونَ
70:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.

70:36 فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ
70:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?

70:37 عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ
70:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

70:38 أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ
70:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?

70:39 كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ
70:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.

70:40 فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَـٰرِقِ وَٱلْمَغَـٰرِبِ إِنَّا لَقَـٰدِرُونَ
70:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza

70:41 عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
70:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

70:42 فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَـٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
70:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,

70:43 يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ
70:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,

70:44 خَـٰشِعَةً أَبْصَـٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
70:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.